WENGI
walioipata hii taarifa wanashangaa imekuaje ni viungo tu vya binadamu
vimepatikana kwenye kontena zima vikiwa vinaingizwa Kenya? vinakwenda
wapi? kazi yake ni nini?
Taarifa
iliyoripotiwa na Citizen TV Kenya inasema Shehena hii iliyokamatwa
baada ya kupitishwa kwenye bandari ya Mombasa inasemekana imesafirishwa
na Mwanasiasa maarufu ambae kabla ya kukamatwa alisema ilikua na bidhaa
za nyumbani ambapo ilipofika kwenye kituo cha ukaguzi wa mashehena cha
Changamwe ilipatikana na vikaragosi vya mafuvu na mifupa ya binadamu
ndipo amri ikatoka kontena
likamatwe.