Home » Archives for 09/11/13
ALL IN ALL SEHEMU YA KWANZA 1
SEHEMU YA KWANZA
Jua kali la saa 9 lilikuwa linawaka kupita
maelezo, Rashid ni kijana mwenye uchu wa maendeleo alipenda kujituma kama
mtumwa akiwa na lengo la kuishi kama mfalme, wakati huu Rashid alikuwa
kibaruani maeneo ya Raha leo pale linapojengwa ghorofa, hapa palikuwa na
mchanganyiko wa wanaume na wanawake watoto na watu wazima palikuwa na
wakandarasi kutoka India na Tanzania Bara, kila mtu alikuwa akisghulika kufanya kazi aliyopangiwa lakini bado
kulikuwa na unyanyasaji kutoka kwa wasimamizi wao.
“Wewe mpumbavu tena
mzembe kabisa masaa mawili unachanganya mchanga uwo kama umeshindwa kazi ni
bora useme mjinga wewe kuna watu kibao ambao wanatafuta kazi wewe umepata
unaizembea nasema kama huwezi kazi nenda kapakatane na mzee walo nyumbani..” Rashid alitolewa maneno makali
yaliochangayika na matusi ya nguoni.
Lakini bosi……. Rashid
alijaribu kujitetea lakini hafla alikatishwa na bos wake “lakini kitu gani tena hakuna malipo leo mana sjaona la mana ulofanya
tangu asubuhi.” Yule msimamizi aliyekuwa akisimamia kundi la akina Rashid
aliondoka huku akionesha ni mwenye hasira na kumuacha Rashid akiwa ameduwaa.
……..
Baby Madaha nomaaa!! Asaini mkataba wa shillingi million 50 na meneja wa mr Nice Kenya; apewa Audi ya kutembelea.
12:52 AM
•
Mwanadada anayefanya vizuri sana kwenye muziki na
filamu,baby Madaha amelamba bingo ya uhakika na kampuni ya Candy n’
Candy Records Label ya jijini Nairobi iliyomsainisha mkataba msanii
mwingine wa Tanzania Mr.Nice hivi karibuni.
Akizungumza kwa simu na bongomovies leo meneja wa msanii huyo
Joe Kariuki amesema kuwa pamoja na msanii huyo kupewa mkataba huo wa
million hamsini (50) pia wamempa mwanadada huyo gari ya kutembelea ya
kisasa aina ya AUDI TT (pichani) na nyumba kali mitaa kijitonyama jijini Dar es salaam.
Pamoja na hayo pedeshee huyo wa Mr.Nice ambaye ndio mmiliki wa
studio hiyo amesema wanataka kumuhamishia msanii huyo jijini Nairobi
nchini Kenya kwa kipindi cha mwaka mmoja ili afanye nao kazi huko kwani
wamegundua kuwa anakubalika sana nchini humo na wapenzi wa muziki.
Baby madaha ambaye anatarajia kutua nchini leo akitoka Nairobi
pamoja na meneja wake kwa ajili ya kuachia video ya wimbo wake wa
kwanza aliofanya na Label hiyo uitwao (Summer Holiday) ambao umefanywa
huko huko jijini Naironi
Mimi na Lucci “Hatumegani kisela” na Hata kama ni ingekuwa kweli haiwahusu; Jokate afunguka
“....Okay leo nimeamua kupitia page yangu ya
Instagram ku-address the following pressing matters kwenye ulimwengu wa
majungu. 1. Luciano Gadie Tsere is NOT my LOVER and noooo hatumegani
kisela. Na hata kama it were true inakuhusu nini. Sioni ishu. Kwenye
Sanaa kuna kitu kinaitwa kuweka uhalisia. And that's what we did na KAKA
DADA. I respect Lucci. Ni kaka yangu na tunafanya kazi nyingi sana
zinakuja. Kuna watu wanefungua mpaka BBM group to discuss me and Lucci
and this so called affair. Jamani kuliko maneno tufanyeni Kazi
kuendeleza nchi yetu 2. Sijifanyi mtakatifu. Ila najitahidi kufanya
matendo yanayompendeza Mungu. Na kwasababu kama binadamu sina ukamilifu
basi only God can really judge me cause ndio anajua moyo wangu kuliko
binadamu yoyote yule. Ila I'm a pretty good girl to be honest. Najaribu.
Kwa nyinyi walimwengu don't be fooled by my PRETTY BABY FACE I know
what I want, am fierce and I don't take trying to tarnish my image
easily. So kindly don't mess with KIDOTI. Msione mtu mkimya mkajua ndio
wa kumuonea. Still waters run deep 3. Yes there's some guy I'm checking
out. Like any other female I deserve love cause I got so much love to
give hey. So whoever it is tafadhali tusiharibiane kwa maneno maneno.
Have a blessed evening.....!!!..
Subscribe to:
Posts
(
Atom
)