Home » Archives for 09/05/13
Taarifa kutoka Dodoma zinadai kuwa kuna
Askari mmoja ambaye ni miongoni mwa walinzi wa Bunge ameenda kufungua
faili Polisi Dodoma na kusema kuwa ametishiwa kupigwa na Mbunge Sugu...
Baada ya kufungua Jalada hilo polisi
wamechukua Difenda 6 na wameingia mitaani kumtafuta ili awekwe ndani
mpaka kesho ndio afikishwe mahakamani asubuhi.
Baada ya kuachia video yake mpya iliyofanywa kwa
gharama ya takribani milioni arobaini na tano za kitanzania,
mwanamuziki wa muziki wa kizazi kipya Diamond Platnumz amefananishwa na
marehemu Steven kanumba kwa jinsi anavyothubutu kufanya mambo makubwa
kukuza Sanaa na kipaji chake tofauti na wasanii wengine wenye majina
makubwa nchini.
Hayo yameongelewa na Msanii dully sykes katika mahojiano yake na mtandao wa Bongo5
hii leo... Katika interview hiyo Dully amemuelezea marehemu kanumba
kama ni mtu aliyethubutu kutumia nguvu, hali na mali, kwa ajili tuu ta
kukuza jina lake kitu ambacho ni nadra sana kwa wasanii hasa wa
Tanzania.
“Kanumba alikuwa ana uwezo wa hata kuchukua nauli yake ya kwenda
sehemu kama Ghana kwenye tamasha la movie lakini ilimradi
kujitengenezea status yake. Kwahiyo Diamond ni mtu ambaye tayari
ameshajitolea kwaajili ya kuutetea muziki wetu.” Alisema Dully sykes