ZUNGUKA kumbi zote za disko. Hautamuona mwanasoka yoyote wa Tanzania amemshika kiuno mwanamke maarufu (celebrity) katika fani yoyote maarufu kuanzia, filamu, muziki hadi siasa. Na sio hao tu, wanasoka wa Tanzania wanaishi dunia tofauti na wanawake wenye hadhi za juu (high Personalities female)
Wakati David Beckham akihangaika na Victoria Adams, Cristiano Ronaldo akihangaika na mwanamitindo wa Kirusi, Irina Shayk, hali ni tofauti kwa mwanasoka wa Tanzania. Ni nadra kwenda katika klabu ya usiku (Nightclub) na kumkuta Nadir Haroub ‘Cannavaro’ akiwa katika mtoko na Mwanamitindo Flavian Matata. Unajua kwa nini kuna sababu nne kubwa. Kwanza ni umaskini unaowakabili. Hawapo katika kiwango cha kushindana kifedha na mastaa wa fani nyingine ndani ya nchi. Wakati mwanamuziki Diamond anaweza kuingiza sh 30 milioni kwa shoo za mwezi mmoja, inamchukua Mrisho Ngassa miaka miwili ya kusaini mkataba mpya ndipo apate fedha hizo.
Wema Sepetu hawezi kwenda kwa Mrisho Ngassa. Atakim