Home » Archives for 07/19/13
MAAJABU MAZISHI YA BAB'KE JOYCE KIRIA
2:05 AM
•
MAAJABU yameibuka kwenye mazishi ya baba mzazi wa Mtangazaji wa Kipindi
cha Wanawake Live kinachorushwa hewani na Televisheni ya East Africa,
Joyce Kiria, Michael Francis Iwambo Kiria kufuatia kuchimbwa kwa
makaburi mawili, Amani lina mkasa mzima.
Kondoo akichinjwa.
Tukio hilo la ajabu lilitokea kwenye msiba wa mzee huyo, Kata ya
Kibosho, Kijiji cha Dakau, mkoani Kilimanjaro wakati wa maandalizi ya
kuuhifadhi mwili wa merehemu huyo.
MASISTER BANDIA WAKAMATWA NA MADAWA YA KULEVYA
1:44 AM
•
Wanawake
watatu wamekamatwa kwa madai ya kujaribu kusafirisha dawa za kulevya
kupitia uwanja wa ndege wakiwa wamevalia kama masista.
Wasafirishaji
hao walisimamishwa wakati wakiwasili kwenye kituo maarufu cha mapumziko
nchini Colombia, sababu polisi walifikiri kwamba mavazi yao hayakuwa
yakionekana halisia.
Maofisa waligundua kwamba kila mwanamke kati yao alikuwa na zaidi ya kilo 4 za cocaine zikiwa zimefungwa katika miguu yake.
Wakiwaongezea fedheha katika
mashitaka, wasafirishaji hao walipangwa mstari mbele ya waandishi wakiwa
bado wamevalia mavazi yao ya kituko kuficha ukweli.
Wanawake hao watatu, wenye
umri wa miaka 20, 32 na 37, walitua kwa ndege kwenye kisiwa hicho cha
San Andres kutoka Bogota siku ya Jumamosi asubuhi.
Kapteni wa Polisi Oscar Davila
alisema wanawake hao walionekana kama wamechanganyikiwa, na kuongeza
kwamba mfumo wa tabia zao haukuonekana kuwa sahihi.
Pale masista hao bandia
waliposimamishwa na kupekuliwa, walikutwa wakiwa na shehena kubwa ya
cocaine ikiwa imefungwa katika miili yao.
Wote watatu waliangua kilio na
kusisitiza kwamba walitumiwa tu kusafirisha dawa hizo sababu ya
matatizo yao ya kifedha, alisema Davila.
Wanawake hao walikamatwa na kuswekwa rumande kwa mashitaka ya kusafirisha dawa za kulevya.
Dawa hizo zilikadiriwa kuwa na
thamani ya Dola za Marekani 35,000 mtaani, kwa mujibu wa Kamishna wa
Polisi wa mji huo, Jorge Gomez.
"Hawakuwa wafuasi halisi wa
dini, hawakuwa masista," alisema. "Kinyume cha hilo, walikuwa wakitumia
mwanya huo kwa ajili ya kazi hii.
"
San Andres, iliyoko Caribbean
nje ya ufukwe wa Nicaragua, ni moja ya mahali maarufu kabisa nchini
Colombia kwa ajili ya wakazi na watalii.
Hatahivyo, inatumika pia kama
njia kuu ya kupitishia dawa za kulevya kwa ajili ya kusafirisha cocaine
kati ya Colombia bara na Amerika ya Kati
ISMAIL WA KICHEFU CHEFU ALELEZEA MIPANGO YAKE BAADA YA KUJITOA KWENYE KUNDI LA WAVANILLA
1:42 AM
•
SAUTI TAMU ni project yangu mpya ambayo itaweza kuleta mabadiliko yanayoanza kutokea katika music , project hii itakuwa na member wasiozidi watano , orodha hyo MSANII ni Peke yangu (smile), WASOMI Ambao ni washauri wangu Watatu 3 ,Pamoja na manegemant yangu .. Kwa hyo naomba suport zenu wananchi ili 2weze kufikia sehemu nzuri kama walizofikia wenze2 .nawapenda sana AHSANTENI SANA.
HIVI NDIVO FACEBOOK WANAVYOPATA PESA KUPITIA KWAKO
12:12 AM
•
Kuwa na Akaunti ya Facebook ni kwa manufaa yako na manufaa ya Facebook |
Facebook ambayo kwa sasa inapatikana
katika lugha 70 ulimwenguni, ni mtandao wa jamii ambao unaongoza kwa kuwa na
watumiaji wengi zaidi duniani. Wewe na mie kama watumiaji wa Facebook
tunainufaisha kampuni hiyo ya Facebook, kwani kupitia kuitumia kwetu
kunaiwezesha Facebook kuingiza mapato kwa njia ya moja kwa moja au nyingine.
Makala hii inakuchambulia namna
ambavyo Facebook inaingiza "vijisenti" vyake:-
1. Kupitia Matangazo: Kwakuwa inao watumiaji wa mtandao wengi, ni rahisi kwa
Facebook kushawishi watu binafsi na makampuni kutangaza bidhaa zao kupitia aina
mbalimbali za matangazo yanayorushwa hewani na Facebook. Mfano , kampuni
inaweza kudhamini POST yake, ili ionekane kwa watu wengi zaidi na mara nyingi.
Pia kuna matangazo ya biashara ambapo unaweza kutengeneza tangazo lako la
biashara na kulirusha hewani kupitia Ukurasa wako wa Facebook (Facebook
Page). Ili kutengeneza tangazo Facebook, unaweza kuenda sehemu maalum
ukiwa Facebook imeandika
CREATE AN AD.Unahitaji kuwa na Credit Card au
Umejisajili na unayo akaunti ya Paypal ili kuweza kulipia
huduma hii.
Mfano wa Matangazo yanayoipatia fedha facebook |
2. Salio maalum la Facebook (
Facebook Credit)
Ni kama vile unavyonunua salio la
simu yako ili utumie salio hilo kupiga simu, ila kwa Facebook, unaponunua Facebook Credit, ni kwa ajili ya kuweza kutumia
credit hiyo kulipia kucheza Games, au hata kununua vitu katika baadhi ya maduka
yanayouza bidhaa zao ndani ya Facebook.
Unahitaji kuwa na Credit Card au
Umejisajili na unayo akaunti ya Paypal ili kuweza kununua
Facebook Credit.
3. Kupitia Kuuza bidhaa mbalimbali
Facebook inayo huduma ya kuuza
bidhaa mbalimbali kwa mtindo wa "Gift" ambapo wewe mtumiaji unachagua
nani unataka kumnunulia bidhaa , kisha unaenda kwa profile ya huyo unayetaka
kumuuzia bidhaa. Utaona sehemu imeandikwa GIVE GIFT, ukibofya hapo utakutana na
aina mbalimbali za zawadi na maelekezo. Hata hivyo huduma hii ya kutoa zawadi
kwa watu haipataki kwa kila nchi. Inabidi ucheki Profile ya mtu husika
unayetaka kumpa zawadi kuona kama GIVE GIFT ipo katika profile yake.
Subscribe to:
Posts
(
Atom
)