Home » Archives for 06/09/13
WAFAHAMU WASANII WALIOSHINDA TUZO ZA KILL MUSIC AWARDS 2013 ILIYOFANYIKA JUNE 8 PALE MLIMANI CITY
11:58 AM
•
Mrisho Mpoto akikabidhiwa tuzo ya wimbo bora wenye vionjo vya asili "Chocheeni kuni:"
Ben Pol akiwa kwenye stage na tuzo yake ya Mtunzi Bora wa Mashairi Bongo Fleva.
Ben Pol akiwa kwenye stage na tuzo yake ya Mtunzi Bora wa Mashairi Bongo Fleva.
MASHUJAA BAND KALA JEREMIAH NA OMMY DIMPOZ WANG'ARA KTMA
11:53 AM
•
Usiku wa jana ulikuwa ni usiku wa furaha sana kwa Mashujaa Band ambao
waliongoza kwa kuondoka na tuzo nyingi kuliko wasanii wengne. Mashujaa
ambao wanafanya vizuri na wimbo wao wa ''Kidole Risasi'' waliondoka na
kura 5 ikiwa ni pamoja na msanii bora wa kiume band Charz Baba, mtunzi
bora a mashari ya band Charz Baba, rapper bora wa band Furguson, wimbo
bora wa band Risasi Kidole na tuzo ya tano waliichukuwa kupitia category
ya band bora ya mwaka huku wakiwatupa kule Twanga Pepeta, Mapacha
Watatu na Msondo Ngoma
EXCLUSIVE MSIKILIZE DIAMOND AKIELEZEA SABABU YA JANA KUTOHUDHURIA TUZO ZA KILIMANJARO
11:41 AM
•
Hitmaker Diamond Platnumz jana hakuweza kuhudhuria tuzo za Kili licha ya
kushinda tuzo mbili kubwa zilizopokelewa na watu wengine kwa niaba
yake. Diamond amezungumza na Bongo5 kueleza sababu iliyomsababisha
ashindwe kwenda kupokea tuzo zake mwenyewe.
Amesema alishindwa kwenda kwenye kilele cha tuzo hizo kubwa nchini
zilizotolewa jana kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam
kwakuwa alitakiwa kwenda kwenye uzinduzi wa kinywaji kipya cha kampuni
ni ya Cocacola, kiitwacho Novida uliofanyika jana usiku kwenye mgahawa
wa Akemi uliopo kwenye jengo la Golden Jubelee, jijini Dar.
Amesema akiwa kama balozi wa Cocacola ilikuwa ni lazima ahudhuria
uzinduzi huo. Diamond alishinda tuzo mbili ikiwemo kubwa ya msanii bora
wa kiume.Msikilize zaidi hapa ambapo anawashukuru pia waliompigia kura
Subscribe to:
Posts
(
Atom
)