Home » Archives for 01/29/13
H-Baba awashangaa mastaa wanaoomba chipukizi pesa kufanya collabo, anakuja na DVD ya show zake na 'Funga zipu'
7:55 AM
•
Hamisi Baba a.k.a H-Baba amewashangaa wasanii wakubwa
waliotoka wanaotangaza kuwa bila kulipwa kiasi flani cha pesa hawawezi kufanya
wimbo wa kushirikishwa na wasanii chipukizi.
'Poteza hit maker' alifunguka katika interview aliyofanya na
Josefly wa radio victoria fm baada ya kuulizwa yeye anahitaji kiasi gani
kufanya collabo na msanii mchanga a.k.a chipukizzi.
"Hebu nambie msanii anakwambia eti kuimba na underground
eti anataka hela! We muulize yeye wakati anataka kutoka nani alimuomba hela?
Hivi huyo underground mwenyewe hela ya studio tu laki moja tu anakosa, halafu
wewe unamuomba sijui millioni tano, anatoa wapi!?"
H-Baba alisema kwa kuwa bado yeye ni mkali wa stage, anataka
kudhihirisha hilo kwa vitendo na hivi karibuni anatarajia kuachia DVD ya
concert kibao alizopiga zikiwemo show alizopiga na wakali kama Koffi Olomide
toka Congo.
Mkali huyo ambae anaaminika sana kwa kuja na idea 'unique'
kwa ngoma anazoachia, amesema amejipanga kuachia ngoma yae mpya inayoitwa
'Funga Zipu' ambayo anaamini itauwa zawadi tosha kwa fans wake.
H-baba alitahadharisha kuwa TRA wawe makini wanapochukua
pesa za wasanii wakati hawawezi kudhibiti wizi wa kazi za wasanii, na kwa
kwamba ingebidi serikali ingetengeneza sheria ya kumlinda msanii kabla
hawajawaza kuchukua pesa kutoka kwenye kazi zao. Akakazia "Wasanii
wanahangaika kweli".
Rick Ross anusurika kifo baada ya kukoswa na risasi 20! Hasimu wake 50 Cent asema kitu kuhusu tukio hilo
7:49 AM
•
Big boss wa MayBach Music Group, Rick Ross amenusurika
kupoteza uhai wake baada ya gari lake aina ya Rolls Royce kukoswakoswa na
risasi kadhaa jana katika mitaa ya Laudedale Florida.
Rosay alikutana na tukio hilo baya wakati ikiwa ni birthday
yake ambapo baada ya kusikia milio ya risasi iliyokuwa inaelekezwa kwenye gari
lao, dereva wa gari hilo alijitahidi kukwepa na kuelekea upande ambao gari hilo
lingekwepa risasi na mwisho kuuvamia ukuta wa jengo moja.
Polisi wa jiji hilo walithibitisha kutokea kwa tukio hilo,
lakini hakuna risasi hata moja iliyolitoboa gari hilo na wote waliokuwa kwenye
gari hilo wako salama kabisa.
Bado haijajulikana nani ambae atakuwa amehusika na tukio
hilo, Rosay aliwahi kupokea vitisho vya kuuawa wakati anapanga kufanya ziara
yake, hata hivyo aliahirisha ziara hiyo japo alisema sio kwa sababu ya vitisho
hivyo.
Rick Ross mwenyewe hajasema kitu kuhusiana na tukio hilo,
lakini hasimu wake 50 Cent yeye anaamini kuwa hilo ni tukio la kujipangia tu.
50 Cent amepost kwenye Instagram picha ya gari la ajai hiyo na kuandika,
"Hahaha fat boy hit the building? lol it looks stage to me. No hole's in
da car."
50 Cent na Rick Ross wamekuwa hawaelewani tangu mwaka 2009.
Subscribe to:
Posts
(
Atom
)