Home » Archives for 01/22/13
Noise Maker kwa DX ni kituo muhimu cha Roma akiwa Arusha, asema anapenda kufanya kazi na wasanii wa A.City.
12:31 PM
•
Wengi waliousikia wimbo wa Roma wa 2030 walipata hisia kuwa
kulikuwa na punch kwa A.City artists Over Tanga ambapo ndo sehemu anakotokea,
ama waliposikia mistari kwenye mashairi ya wimbo wake mmoja akisema 'Hip Hop
ina uwanja mpana usiseme tu iko R-Chuga'. Kama wewe ni mmoja wao utakuwa
unakosea hivi na inabidi umsome tena Roma.
Hivi ndivyo alivyosema Roma kupitia ukurasa wake wa facebook
na kuambatanisha na picha akiwa na Mo Plus na Banx Baba la Ukoo.
"KILA NIENDAPO ARUSHA (ARACHUGA)!!! HUPENDA KUFANYA
NGOMA NA MANINJA WA KULE!! DX HUSIMAMIA MIZIGO YOTE HII
with ma ninja BAAAANXXXX na MO PLUS BABA LA UKOO
NGOMA INAITWA "UKWELI"
A.city "
R.O.M.A (Rhymes Of Magic Atraction) ndivyo anavyojiita na
kulitafsiri jina lake, kila akitoa wimbo mashairi yake huwa na nguvu ya ajabu
kuvuta attention ya wasikilizaji wake kitu ambacho kimesababisha watu wengi
kuvutika na kununua wimbo wake 2030 kwa shillingi 3000 kwa njia ya email,
lakini pia baada ya kuuachia tu uliongoza kwa kupakuliwa kwenye mtandao kwa
hapa Tanzania.
New Video: Rick Ross aachia video ya wimbo wake aliyoi-direct mwenyewe "Pirates
12:22 PM
•
Big boss wa Maybach Music Group Rick Ross ameachia video ya
wimbo wake 'Pirates', uliopo kwenye album yake ambayo ilikuwa nominated kwenye
tuzo za Grammy "God Forgives, I Dont".
Rick Ross mwenyewe ameshiriki katika kuiongoza video hiyo
kama co-director akishirikiana na muongozaji maarufu wa video Dre Film ambae ni
mshika kamera wa Maybach Music Group. Video imefanyika Miami, Florida ikiwa na
story nzuri.
Iangalie hapa:
Justin Bieber hajapenda mama yake kufanya project ya filamu ya kupinga utoaji mimba.
12:10 PM
•
Siku chache baada ya mama mzazi wa mkali wa pop na R&B
Justin Bieber kutangaza kuwa anatengeneza filamu fupi ya kupinga utoaji mimba
(anti-arbotion), inasemekana kuwa Justin Bieber hajapenda project hiyo mpya ya
mama yake.
Kwa mujibu wa Chicago Sun Times, mwimbaji huyo mwenye umri
mdogo hajapenda project hiyo kwa sababu imebeba mambo ya kisiasa.
Mama yake Bieber Pattie Mallette alitangaza hivi karibuni
kuja na project mpya ya filamu inayoitwa "Crescendo" inayopinga
utoaji mimba, akiwa na lengo la kuwahamasisha vijana kufahamu kwamba kuna
sehemu ya kwenda ambapo watu watawatunza na sehemu ya kuishi kama watapata
ujauzito na wakaona hawana sehemu ya kuegemea.
Crescendo inatarajiwa kuoneshwa kwa mara ya kwanza february
28,na waandaaji wa filamu hiyo wamepanga kukusanya pesa kiasi cha $10 million
kwa ajili ya vituo vya kuwahudumia wajawazito.
Subscribe to:
Posts
(
Atom
)