Kuprove kwamba yeye ni mkali hakuhitaji maneno bali vitendo,
hiki ndicho rapper wa kike wa YMCMB ameonesha. Baada ya kuachia list ya track
27 zitakazokuwa kwenye album yake mpya Pink Friday:Roman Reloaded-The Re-Up,
sasa ameachia ngoma moja toka kwenye album hiyo itakayokuwa na CD mbili na
wakali kibao wamepewa shavu kuinogesha.
Fredom ndo jina la track hiyo na humo kweli kaonesha ukali
sio kurap tu lakini hata kuimba pia anaweza.
Kwenye track hiyo Nick Minaj anajaribu kukumbuka enzi zake
wakati anaanza kuingia katika ulimwengu wa muziki na kuwashukuru watu
waliomsaidia kuvuka mambo kibao na kufika hapo alipo sasa. Lakini kama kawaida
Rapper huyo wa kike hakuacha kuwachana wale ambao walikuwa wanajaribu
kumrudisha nyuma ama kumchukulia poa.
“I feel free / I feel freedom / why they mad?/ You should
see them. It’s crazy in her,” anafunguka Minaj kwenye chorus.
Minaj ametema mistari ya kujisifu kama kawaida tena kwa
mitambao mizuri sana, “Freedom” ni ngoma ambayo inaonekana kupokelewa vizuri na
fans wake na inatarajiwa kuanza kuchezwa kwenye vituo mbalimbali vya radio hasa
hasa vipindi vya pop na hip hop.
“Pink Friday:Roman Reloaded-The Re-Up” itakuwa dukani na
inaweza kununuliwa kwa kudownload kwenye iTunes.