NEW VIDEO: KAGOMAZ - FILANGE

10:34 AM

Akon amsaini Konvict mtoto wa mtaani kutoka kenya mwenye miaka 14, story yao ni kama movie.

10:33 AM

Wiki hii imeanza na zali zaidi ya lile la mentali kwa mtoto ambae alikuwa anaishi katika mazingira magumu sana nchini Kenya, inaweza kuwa ndoto alizoota zikmekuwa kweli na kama hakuwahi kuota basi Mungu amemsapraiz na kujikuta anapata deal la uhakika la kufanya muziki chini ya lebel kubwa duniani ya ‘Konvict’.
Mtoto huyo anaeitwa Wilson alimsimamisha Akon wakati anaelekea kupiga show pande hizo na akaona kabisa kuwa hii ilikuwa ni chance ya yeye kumueleza Akon ya moyoni tena sio kumuomba mkwanja ila ni kumuomba kujiunga na lebel ya Konvict. Duh, unaweza kudhani mtoto huyo alikuwa mwehu eeeh…dogo alirusha mkuki vizuri!!
Baada ya Akon kukubali kusimama tu mtoto huyo alizitumia dakika chache kumsimulia hali mbaya ya maisha anayoishi na jinsi ambavyo baba yake alivyomtesa na kulazimika kulala nje, akaeleza jinsi gani anavyoupenda muziki na hana jinsi ya kuweza kuingia studio kurekodi. Surprisingly, Akon akaamua kumpa nafasi, akaingia nae kwenye gari lake na wakaelekea wote kwenye concert yake.
Hatujui nini kiliendelea kwenye gari lakini inaonekana waliendelea kuongea kuhusu yale waliyoyaanzisha. Na haikuwa raisi kwa Akon kumpa nafasi kirahisirahisi tu.
Wakati anaendelea na performance yake mkali huyo toka Senegal alimuita stejini yule mtoto. Kwa mara ya kwanza kwenye jukwaa kubwa na Akon, dah, hii ni bahati ama baraka?! Akon akamkabidhi dogo mic na kumwambia aperform!
Ni kama ulikuwa mtihani wa mwisho kwa dogo huyo ambao ungemtoa lawama Akon kirahisi, dogo alifunika vibaya na kuonesha kipaji kikubwa alichonacho.
Haikuhitaji press release ama press conference kutangaza uamuzi wa Akon, alishika mic na kutangaza mbele ya umati wa watu, “Wilson the newest member of the Konvict family”. Ni hivyo tu dogo anachukua pipa kwenda kuishi ndoto zake Marekani.
Huyu ni mtoto wa kiafrika mwenye story ya mafanikio inayofanana na ya Akon.

NEW VIDEO: GELLY WA RHYMEZ - MEMORIES

10:32 AM

Hereni za kumsapoti Obama alizovaa Beyonce zampa deal mtengenezaji, aongeza mauzo ya hereni kwa kasi, apata order dunia nzima.

10:31 AM

Ni usanii na ubunifu uliofanywa na designer mmoja wa mambo jewelries aliyetengeneza hereni ambazo wanawake walitakiwa kuzivaa ili kuonesha kuwa wanamsapoti Barack Obama katika uchaguzi wa uraisi wa Marekani, ambae aliuza kidogo sana mwanzoni lakini mambo yamebadilika mara tu baada ya Diva Beyonce kuzivaa hereni hizo.

Beyonce akiwa amevaa hereni hizo
Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ designer huyo anaeitwa Erika Pena amesema tangu azitengeneze alikuwa ameuza pea 5 tu lakini tangu Beyonce azivae hereni hizo jumamosi iliyopita ameshauza pea 1,300 na anazidi kupata order kutoka sehemu mbali mbali duniani ikiwa ni pamoja na Uingereza, Uswizi, Chile, na Argentina, lakini order kubwa sana inatokea Uingereza.
Bei ya pea moja ya hereni hizo ni dola 32…ambazo ni karibia 50,000 za kibongo.

NEW VIDEO: JOH MAKINI FT. DUNGA - SIJUTII (Official Music Video)

10:30 AM

New Video: Luten Kalama ft. Neibour - Kama Nani ( Official Music Video)

10:27 AM

NEW TRACK: AY ft. V - MONEY

10:23 AM

Rihanna na Karrueche wanaona poa kuchangia penzi la Chis Brown!

10:16 AM

Mkasa wa mapenzi yenye pembe tatu zinazowahusisha warembo wawili Rihanna na Karrueche Tran kwa 'Don’t wake me up' hit maker Chris Brown unazidi kunoga siku hadi siku na imesemekana kuwa warembo hao wako poa tu na maisha yao na ‘baby boy’ wao Chris Breezy.
Mtu mmoja ameiambia Hollywood Life, “he got them both twisted up. He is trying to get as much p-y as he can before he leaves next month.”
Chanzo hicho kiliendelea kufunguka, “Chris anawapenda kweli wote na wanajua hilo na wao wanampenda pia”, akaendelea, “it’s crazy situation. Na inafanya kazi kwao, na ni kama RiRi na K.T wako poa tu na hili, hivo ndivyo ilivyo.”
Lakini stori za mtaa kwa upande mwingine zilisema Rihanna aliogopa pale alihisi kuwa labda Chris angeenda na Karrueche T kwenye party yake kubwa ya Halloween iliyowakutanisha mastaa kibao jumatano ya wiki hii.
Mtu mmoja alisema, “ingawa the 'umbrella' hit maker RiRi alikuwa poa tu kwa kile kinachoendelea kati ya Chris B na K.T lakini hakuwa na uhakika kama Chris ataamua kwenda kwenye party yake na K.T na hii ni kutokanana tetesi ambazo zilikuwa zimetapakaa mitaani na kwenye mitandao kuwa huenda Chris akatokea pale akiwa na K.T kama kawaida. Hapo ndo utaona kweli mapenzi ya watatu hayawezekani hasa inapoonekana kuwa itabidi kukutana kwenye eneo moja.
Chis Brezzy alitangaza kuachana na Karrueche October 4, na kauli yake ilikuwa ,” nimeamua kuwa single ili nifocus kwenye kazi yangu. Nampenda sana Karrueche lakini sitaki kumuona anaoumia kwa sababu ya urafiki wangu na Rihanna. Badala yake inabidi niwe single ili Kurusu kila mmoja wetu kuwa na furaha.”
Siku chache zilizofuata Chris B alitoa video ikiwa na kauli nyingine inayoonesha kweli anawapenda wote Rihanna na Karueche na hajui afanye nini na hajui kama kweli inawezekana kuwapenda watu wawili lakini ndivyo yeye anavyojisikia, lakini mwisho wa siku ikaonekana kabisa ameamua kuhamia rasmi kwa Rihanna wake wa zamani na kumtangaza rasmi japo ndo hivyo tena hawaachani na Karrueche pia. 

Haya ndiyo yanayoitwa Triangular Love, “mapenzi ya pembe tatu”.

NIMEGUNDUA VITU VINGI KWENYE HII SHOW HEBU NAWE ANGALIA UTAGUNDUA KITU GANI

10:12 AM

BEHIND THE SCENES YA TAMTHILIA YADI SEHEM YA 45

10:05 AM










































 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates