WASANII MBALIMBALI WAFUNGUKA ISHU YA LORD AYES POLISI NAO WATHIBITISHA KUMSHIKIRIA

1:20 PM



 Kamanda wa Polisi mkoa wa kipolisi wa Kinondoni Charles Kenyela amethibitisha jeshi lake kumshikilia msanii Lord Eyes ambae toka weekend iliyopita taarifa zake zimesambaa baada ya kushutumiwa kuhusika na wizi wa vifaa mbalimbali kwenye gari la mwimbaji Ommy Dimpoz.
Namkariri Charles Kenyela akisema “ni kweli Isaac Waziri Maputo mwenye umri wa miaka 28 alikamatwa tarehe 20 mwezi wa kumi usiku maeneo ya Kinondoni, kukamatwa kwa mtuhumiwa huyu ni kutokana na taarifa tulizozipata kupitia kwa binti mmoja aitwae Kurushinde Hillary (22) mwenye asili ya kiburushi lakini mkazi wa Mwananyamala kwa Makoma Dar es salaam, alikamatwa siku hiyo hiyo kabla ya Lord Eyes”

“Alikamatwa kuhusiana na matukio ya wizi kwenye magari yani kuna mtindo ambao umeibuka ambapo ukipaki gari yako gari nyingine ya wezi inakuja inapaki jirani na gari yako ambapo kwa muda mfupi wanafanya utundu wao wanaoujua, wanafungua gari na kuiba mali iliyoko ndani, mara baada ya huyu binti kukamatwa katika kuhojiwa mtandao wake anaoshirikiana nao alimtaja mtuhumiwa Isaac Waziri Maputo (Lord Eyes)” – Kamanda Kenyela
Kwenye sentensi nyingine Kamanda Kenyela amesema “watu wengi wamelalamika kuibiwa laptop zao, mabegi, mifuko na hata silaha kwa maana mtu anakua anajiamini anaacha kwenye gari akiamini kwamba ameshalock lakini watu hawa na mtandao wao wamekua ni hatari kiasi kwamba wameliza watu wengi”
“Watuhumiwa hawa wawili Kurushinde na Lord Eyes tunawashikilia kwa tuhuma zipatazo 30, yani matukio mbalimbali 30 pengine yanaweza yakaongezeka ambayo yameripotiwa kutokea katika maeneo mbalimbali kama vile Mlimani City, Kijitonyama, ufukwe wa bahari kama Coco beach, kwenye kumbi mbalimbali za starehe na pia  kwenye maeneo ambayo kunakua na harusi, sehemu ambazo kunakua na magari mengi watu hawa ndio huwa wanaitumia hiyo nafasi kufanya uhalifu, tunawashikilia kwa makosa ya wizi”

  KUHUSIANA NA TUHUMA ZA WIZI ZINAZOMKABILI MSANII LORD EYES LIMEPOKELEWA TOFAUTI TOFAUTI NA WASANII WENZAKE:
 
1:C PWAA ameandika jana kupitia ACC yake ya FB ,akishauri WASANII hao wawili kusameheana,kwa mkosaji kukubali kosa kama amehusika na mkosewa kusamehe kwa masharti nafuu ili AMANI iweze kutawala.
2-RAMA DEE Leo ameandika kupitia kurasa yake ya FB KWA MAWAZO tofa
uti kidogo kwa kuanza kumkandia LORD EYES kwa kuendekeza tabia zake za uvutaji madawa ya kulevya:LORD EYES uwe umeiba ama hujaiba kutokana na tabia za utumiaji MADAWA YA KULEVYA,lazima utahusishwa na mambo kama hayo ya wizi,nakuongeza"MCHIZI GARI LIMEWAKA ANAHITAJI MSAADA,HALI YAKE NI MBAYA,Pia kwa ANGALIZO RAMA DEE anasema kama ushahidi utadhihirisha LORD hajaiba OMMY DIMPOZ juwa SHOW zake zitaishia CHALINZE Pale ARUSHA baadae sana.


OMMY DIMPOZ naye ameandika kupitia ukurasa wake wa TWITTER leo akidai kinachomuuma LORD EYES alidhamiria coz GARI yangu anaijuwa na MIZINGA huwa akinipiga huwa namtoa...

 

 
Msemaji wa kundi la Weusi Nikki wa Pili ametoa kauli ya kwanza toka kukamatwa kwa Lord Eyez wa kundi hilo kwa tuhuma za wizi wa vifaa vya gari la Ommy Dimpoz.
Namkariri Nikki wa Pili akisema “kwanza hiyo ni habari ya ghafla alafu ni ya kusikitisha na kushtua, ni habari ambayo imetupa shida na mpaka sasa inatupa shida sana kwa sababu watu wengi wanatupigia simu kutuuliza inakuaje”
“Ukiangalia kwenye mitandao ya facebook na twitter kote imesambaa, unajua ukijua ukweli ni kitu cha msingi sana kwa sababu sisi pia tulikua hatufahamu kilichotokea, kwa hiyo cha kwanza tulichokifanya ni kutaka kujua kilichotokea, mfano mimi niliona kwenye mitandao kwamba Lord Eyes amekamatwa kwenye eneo la tukio yupo kwenye gari lakini kufatilia nikaja kugundua haikua eneo la tukio na sio gari hilo,  uhalifu ulifanyika alhamis na alikamatwa jumamosi” – Nikki wa Pili
“Kitu cha busara tulichoamua kufanya tumeamua kufatilia kisheria ili tujue uhalisia ni upi ili tuweze kutoa tamko kwa sababu sisi wenyewe Lord Eyez hatujamuona wala hatujaongea nae, na kingine ambacho kinasikitisha ni kwamba Lord Eyez ndio ametuhumiwa kama mtu binafsi lakini ukiangalia kwenye mitandao watu wanawashambulia weusi kitu ambacho sio sahihi kabisa, mimi Joh Makini, Bonta, G Nako tumepokea hiyo habari kama mtu mwingine yeyote” – Nikki wa Pili.

 duuuh WHAT REAL SITUATION-POLICE WE NEED 2 KNOW DA TRUTH.....
 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates