Presenter anae fanya vizuri kisiwa zanzibar toka Hits fm Radio, 2POINT amefunguka kuhusu mahusiano yake na mwana dada toka bongo movie SHILOLE msikilize 2POINT akiongea na chiwileinc
Home » Archives for 10/03/12
Nick Minaj ambwatukia Mariah Carey, amtishia “I’m gonna knock you out”
1:55 PM
•
Nick Minaj |
Wiki chache baada ya Mariah Carey kukanusha
tetesi kuwa alikuwa na beef na Young Money Queen Nick Minaj ambae ni jaji
mwenzake kwenye American Idol sasa mambo yamekuwa tofauti baada ya video yenye
picha tofauti kabisa na kile kilichoelezwa na Carey kusambaa kwenye mitandao.
Video hiyo inaonesha Nick Minaj akiwa
kakasirika na anampa makavu live Mariah Carey, tukio hili limetokea wakati
wanaendelea na kazi yao ya kujaji washiriki mbalimbali na safari hii walikuwa
Charlotte, North Carolina.
Mtu mmoja ambae alishuhudia live tukio hilo
amesema kuwa Nick Minaj alionekana kupandisha mzuka na kufikia hatua ya
kumtishia the R&B diva Mariah Carey na kusema “I’m gonna knock you out”.
Chanzo hicho kiliendelea kusema kuwa Nick
Minaj aliongea kwa sauti ya juu sana na kumtolea matusi makali Mariah Carey
akisema “I told them, I’m not f***kin’
putting her f**kin’ highness there.” Lakini hii sehemu haikushikwa na lensi ya
camera hiyo iliyokuwa inachukua matukio ya American Idol.
Inasemekana kuwa hii varangati ilitokea
baada ya kutofoutiana sana katika maamuzi kwa washiriki walio-perform siku
hiyo. Wakati hayo yanatokea, Nick Minaj na Mariah Carey walikuwa wamekaa kwenye
meza ya majaji, na jaji mwenzao Keith akiwa amekaa katikati yao na Randy
Jackson akiwa amekaa mwishoni upande wa Mariah Carey.
Kutokana na hali hiyo watayarishaji wa
American Idol iliwalazimu kusimamisha performance ya siku hiyo ili majaji hawa
wacool down kwanza. Hali hii inaonekana kuwatishia waandaji wa American Idol na
wana wasiwasi kama Nick Minaj na Mariah Carey watadumu kwa muda mrefu wakiwa
wanafanya kazi yao pamoja kama majaji wa American Idol.
Mariah Carey |
Katikati ya mwezi September iliripotiwa
kuwa Nick Minaj na Mariah Carey hawana maelewano mazuri, na mtu mmoja ambae ni
mfatiliaji wa mambo ya muziki Marekani alisema hata Mariah Carey alipopigiwa
simu kuambiwa kuwa Nick Minaj ndo atakuwa jaji mwenzake kati ya wale wanne
alikata simu.
Lakini September 17 ambapo MTV ilienda New
York pale ambapo American Idol ilikuwa imeanza na ikafanyika kwa siku mbili,
ili kujionea nini kilikuwa kinaendelea kati ya Mariah Carey na Nick Minaj, na
walipouliza kuhusu kutoelewana, wote walikuwa wanatabasamu kama vile walisikia
utani hivi, na Mariah Carey akaonesha kushangazwa na taarifa hizi jinsi
zilivyosambaa kwa haraka ndani ya muda mfupi sana, na akamaliza kwa kusema
"It's fun, it's music, it's singing, it's laughter," na Nick Minaj
akawa anatikisa kichwa kuonesha anasapoti alichokuwa anasema Mariah Carey.
Wajuzi wa mambo walisema time will tell
sasa kila kitu kinaanza kuonekana hadharani, chanzo kabisa cha kutoelewana kwa
wawili hawa bado hakijajulikana kwa sababu kama Mariah Carey alikata simu pale
tu aliposikia jaji mwenzake atakuwa Nick Minaj, basi chanzo sio kutoelewana
katika maamuzi ya ujaji wao, there must be a long term factor.
Britney Spears, Taylor swift wamsogelea Oprah katika list ya wanawake wanaolipwa zaidi, Rihanna nafasi ya nne, Beyonce afichwa.
1:53 PM
•
Oprah Winfrey |
List ya wanawake wanaojihusisha na entertainment
wanaolipwa mpunga mrefu zaidi duniani kwa ajili ya kazi zao kwa mwaka
iliyotolewa na Forbes inaonesha kuwa Oprah Winfrey anayeendesha talk show
anashikilia nafasi ya kwanza, ambapo kati ya may 2011 na may 2012 amepokea $
165 million. Na imegundulika kuwa bado kuna mshahara mwingine hajapata, kwa
hiyo hautajumuishwa kwenye pato la mwaka ujao, 2013 ili isiwe nafasi ya
kumuongezea ushindi tena mwaka ujao kumbe kuna pato la mwaka huu bado
analisubiria.
Britney Spears |
Katika list hiyo nafasi ya pili imekamatwa
na judge wa X Factor mwanadada Britney Spears, ambae yeye ameingiza mpunga wa
ukweli kiasi cha $58 million ndani ya mwaka mmoja. Kwa mujibu wa Forbes Spears
alimake mkwanja mrefu sana kupitia album yake na hasa kupitia tour ya album hiyo
aliyoibatiza “Femme Fatale tour”, na
alijazilishia kwa mkataba mnono wa kuendesha X Factor ambao ni $15
alizozisign.
Taylor Swift |
Nafasi ya tatu imekamatwa na mwanadada
Taylor Swift ambae ana historia ya aina yake na MTV VMAs, alipovamiwa jukwaani
na Kanye West, na hili tukio liliwafanya watu wengi zaidi kutega masikio kwa
huyu mwanadada mwenye umri wa miaka 22 hivi. Yeye amemfata kwa karibu sana
Briteney Spears kwa kuingiza $57 millioni kwa mwaka kama pato halisi. Huyu ni
mwanadada mwenye umri mdogo zaidi kwenye hii list na tour yake ya Speak Now
ilichangia kwa kiasi kikubwa sana pato lake lakini pia ngoma kibao kali
alizoachia ikiwemo ile safe &sound. Na mwezi huu anatarajia kuachia album
yake inayoitwa Red. Kumbuka wimbo wake wa kwanza ulikaa kwenye nafasi za juu sana
za Billboard’s Hot 100 chart kwa muda wa wiki tatu.
Rihanna |
Nafasi ya nne imekamatwa na the R&B
Queen Rihanna, lakini hapa amefungana na mwanadada Ellen DeGeneres wote wakiwa
wameingiza kiasi cha $53 million.
Nafasi ya tano imekatwa na Lady Gaga
na jaji wa zamani wa American pop Idol
Jeniffer Lopez, wakali hawa wamefungana pia na wameingiza mpunga kiasi cha $52
million kwa kipindi cha mwaka mmoja. Gaga album yake iliyoambatana na tour ya
Born This Way imemsaidia kufika hapo.
Wakati majina yanaendelea kushuka, list
ilifungwa na supper modal Gisele Bundchen ($45 million) Katy Perry ($45
million) na Judge Judy wa TV show ($45 million).
EXCLUSIVE: NEW VIDEO: C-SIR MADINI - PAIN KILLER (Official Video)
1:45 PM
•
C-sir Madini |
Wimbo huu umeandikwa na kua produced na Kid bwoy wa Tetemesha Recordz. Video imesimamiwa na Adam Juma wa Visual Lab/Next Level.
Kwa mujibu wa management ya C-sir video itaanza kuonekana katika vituo vya TV mapema wiki Ijayo, na itaanza kusikika katika vituo vya radio wiki moja baada ya kuanza kuruka katika Tv stations.
Diamond Platnumz apata management mpya, shows, mavazi, matangazo, vyote vitasimamiwa na I-VIEW MEDIA.
1:39 PM
•
Mkurugenzi wa I-View Media Raqey na Diamond wakisaini mkataba |
Baada ya zoezi la kusign contract ya miaka miwili, sasa kampuni ya I-View Media ndio itashughulika moja kwa moja na upokeaji wa bookings na kunegotiate deals zote za msanii Diamond za ndani na nje.
Hii ni hatua nzuri sana kwa Diamond, sababu hakuna biashara inayofanikiwa bila kuwa na miongozo mizuri ambayo inasimamiwa na watu professionals wa field husika.
Hongera sana Diamond kwa hatua hii muhimu katika career yako.
Subscribe to:
Posts
(
Atom
)