Home » Archives for 09/15/12
Witness aja na solution kwa matatizo ya nguvu za kiume
5:36 AM
•
Marafiki wa rapper wa kike nchini, Witness kupitia Facebook
husasani wale wa kiume, wamepata somo la bure la jinsi la kuongeza nguvu za
kiume.
Hivi ndivyo alivyoandika:
Tsup my pipo, leo ninapenda kutumia facebook vizuri kwa
kuzungumzia kazi ya madini ya zinc mwilini na yana patikana katika vyakula vya
aina gani na yanaweza kuwa destroyed madini ya zinc yanapatikana haswa
kwnye,cereals,nyama aina ya offal,kaa,pweza,ngisi,maharagwe,yeast,uyoga,mbegu
za maboga alizeti pamoja na karanga korosho haswa brazilian nuts ina saidia sna
kutibu vidonda naturally ndo maana watu wnye madini ya kutosha ya zinc mwililni
huwa wanapona haraka kuliko wengine kwa kuwa miiili yetu iliumbwa kujiponya
yenyewe, endapo ukaipa lishe bora vitamins na minerals za kutosha, pia husaidia
kwenye mental alertness,ngozi kufunctioni zuri hata vichunusi meno na pia
husaidia watu wenye matatizo ya manii kama ni ndogo na kushindwa kuzalisha
mbegu za kutosha, huongeza uwezo na hamu ya kuchuja nafaka kwa wanaume na
wanawake na kuongeza ufanisi wa afya ya viungo vya uzazi na endapo madini haya
yakiongezwa na vitamins za nyingine yanaweza kutumika kwa kuondolea sumu
mwilini na kusaidia mfumo wa chakula kufunction vizuri.
Maisha Plus 2012 yaendelea na usaili
5:34 AM
•
Kaka Bonda, Kipanya na Mwanahamisi wakiwa redioni |
Baada ya kukamilisha usaili Dodoma, Kahama,
Kagera,Singida, Mwanza, Morogoro, Iringa sasa usaili unaelekea mkoani Mbeya
ambapo utafanyika Sept 15 .
Crew nzima ya Maisha Plus/Mama Shujaa wa
Chakula inayodhaminiwa na banki ya NMB na Oxfam baada ya hapo itaendelea na safari kutoka
Mbeya moja kwa moja mpaka Kilwa, ambapo itafanya usaili Septemba 17, kesho yake yaani Septemba 18
usaili utaelekea Masasi mkoani Mtwara.
Dada Mwanahamisi akiongea na vijana |
Septemba 20 itakuwa zamu ya Wanzanzibar
kusailiwa katika kumpata mwakilishi wa Maisha Plus kisha timu itarejea Dar tayari kwa usaili
ambao utafanyika Septemba 22 na 23.
Kitakachofuata baada ya usaili wa Dar ni
kipindi cha Maisha Plus/Mama Shujaa wa Chakula kuanza kuonekana kwenye runinga
yako. Usikae mbali na TBC1 kwasababu ndiyo itakayokusafirisha nchi nzima ukiwa kwenye sofa lako nyumbani.
Team iliyojitolea kuingia msituni kutafuta vijana watakaoingia kijijini |
Kubwa
kuliko
Wakati usaili ukiendelea mikoani hapa nchini,
Huko nchini Burundi nako usaili wa kuwapata washiriki wawili ulikuwa unafanyika
kwa maana hiyo safari hii shindano la Maisha Plus litakuwa na washiriki kutoka
huko.
Huu ni mwanzo wa shindano hili wa
kuzishirikisha nchi zote za Ukanda wa Mashariki ya Afrika.
Kwa wakazi wa Dar fomu za ushiriki
zinapatikana katika duka la Masoud Kipanya lililopo Millenium Tower, Kijitionyama. Unaweza kupata usaidizi ka
kupiga namba hii 0717 710303.
HAPPY BIRTHDAY DOGO JANJA
5:22 AM
•
Leo ni siku ya
kuzaliwa Dogo Janja msanii kutoka Mtanashati Ent, anasema anajisikia poa
sana kutimiza miaka 18 leo na kuingia step nyingine ya maisha.
PIPI AJIFUNGUA MTOTO WA KIUME
5:17 AM
•
Msanii anayetamba na video yake mpya inayoitwa UNAPOKUWA MBALI hapa
namzungumzia PIPI jana usiku alijifungua mtoto wa kiume na kumpa jina la
KINGSTONE
Subscribe to:
Posts
(
Atom
)