MUONEKANO MPYA WA JIJI LA DAR ES SALAAM

8:12 AM

KIRAKIRAMI FT HUNTER B - TOGETHER MP3

7:45 AM
kirakirami
Song: together
Artst: kirakirami ft hunter B
Studio: six records
Producer: side tothelee

KIRAKIRAMI FT BIZZO RHYMES -NAZISAKA DOOH MP3

7:14 AM
kirakirami
Song;: Nazisaka dooh
                 Artst: kirakirami ft bizzo rhymes
Studio: B-records....
  Producer: suma kopa

Ukitaka kujua Hasheem Thabeet ni mrefu angalia picha hii

7:02 AM
Dida akiwa na Hasheem Thabeet

Kim Kardashian atupa nguo zake zote sababu ya Kanye West

6:51 AM


Kanye West anamtaka mpenzi wake Kim Kardashian avae mavazi ya heshima na ya kuvutia.


Katika kipindi cha jana cha Keeping Up With the Kardashians, rapper na mbunifu huyo wa mavazi, 35 – ameweka deal na mpenzi wake huyo wa miezi mitano kuwa kama atazitupa nguo zake zote atamnunulia zingine.

USIKU WA SAUTI ndani ya mikoa 4 Dar es Salaam, Arusha, Mwanza na Zanzibar.

6:45 AM
Na mwandishi wetu:
KIONGOZI wa zamani wa bendi ya Diamond Sound ‘Dar es Salaam Kibinda Nkoi’, Ibonga Katumbi ‘Jesus’ mwezi ujao ataungana na baadhi ya wanamuziki wengine wa kundi hilo katika onyesho la Usiku wa Sauti na Marafiki wa Kweli litakalofanyika katika mikoa ya Dar es Salaam, Arusha, Mwanza na Zanzibar.
Akizungumza mjini Dar es Salaam jana, mratibu wa tamasha hilo Martin Kadinda ‘Single Button’ alisema onyesho hilo linahusisha wanamuziki wakongwe ambao wataungana na Jesus pamoja hao wa Diamond.
“Kila kitu kinaenda sawa aliyekuwa amealikwa kwenye onyesho ni Jesus lakini katika onyesho hilo atatakiwa kuimba nyimbo zake kadhaa ambazo alitamba nazo akiwa Diamond na Beta Musica kwa hali hiyo alishauri aite wenzake ili wamsindikize.
“ Kutokana na heshima walijengeana wenzake walikubali kumsindikiza, kwa hiyo mashabiki wa Kibinda Nkoi baada ya miaka 12 wataweza kuwaona tena Ibonga Katumbi, Richard Mangustino, Wayne Zola Ndonga na Alain Mulumba Kashama wakisimama pamoja na kuimba tena nyimbo zao kali,” alisema Kadinda.
Kadinda alisema lengo kubwa la onyesho hilo ni kuthamini muziki wa zamani na kufundisha matumizi ya vyombo vya muziki.
Katika onyesho hilo pia watakuwepo wapiga magitaa kama Elly Chinyama, Adolph Mbinga, Marcis Mengi na mpiga drum wa mwisho kuipigia Diamond Sound Kata Nyama Serikali.
Baadhi ya nyimbo zitakazopigwa katika onyesho hilo ni pamoja na Neema, Mugheni, Chance, Jetou, Bana Beta, Midabwada na Infarouge.  Kadinda alisema wanamuzki wengine watakaoshiriki kwenye onyesho hilo wataendelea kutangazwa.

THE MAKING OF PAIN KILLER by C-SIR MADINI

6:43 AM
C-sir Madini amemaliza kushot kichupa cha wimbo wake mpya ambao unatarajiwa kutoka mwezi ujao unaoitwa PAIN KILLER. Audio ya wimbo huo imetengenezwa na Kid bwoy wa Tetemesha Recordz, na video imetengenezwa na Adam Juma wa Next Level, na katika video hiyo C-sir amevalishwa na Kidoti Fashion ya Jokate. Fans kaeni tayari kwa ujio huu mpya wa C-sir Madini.

Audition ya Maisha Plus 2012 yaanza

6:40 AM
Awamu ya kwanza  ya zoezi la kwasaka vijana watakaoweza kumudu mchakamchaka wa shindano la Maisha Plus, imeanza jana (Agosti 27) huko Bagamoyo mkoani Pwani.
Leo shindano hilo litafanya usaili katika wilaya ya Lushoto ambako zoezi hili litafanyika katika maeneo ya mjini mwa wilaya hiyo.

Baada ya hapo ratiba za audition zitaendelea kama ifuatavyo;
Agosti 29- Kilimanjaro/ Sanya juu
Usaili utafanyika katika mji wa Bomang’ombe

Agosti 30- Arusha/ Ngorongoro
Usaili utafanyika Karatu

Agosti 31 – Singida
Usaili utafanyika Singida Mjini

Septemba 1- Iramba
Usaili utafanyika Iramba Mjini

Septemba 2- Dodoma
Usaili utafanyika Kondoa Mjini
Hii ni awamu ya kwanza ya usaili wa shindano hili, audition zitaendelea stay tuned kwaajili ya tarehe na mahali ya auditon zitakazoendelea……….
 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates