Home » Archives for 08/02/12
Leona Lewis sasa kurap, amwambia Minaj: 'I'm coming for you Nicki!'
2:05 PM
•
LEONA Lewis ameamua kujaribu bahati yake kwenye rap na
albam yake mpya itakuwa imejaa michano tu.
Na mrembo huyo anajiamini kuwa atakuwa tishio kubwa kwa Nicki
Minaj ambaye hana mpinzani kwa sasa kibiashara.
Mwanamuziki huyo wa Uingereza kwa sasa anamalizia
malizia ngoma yake mpya ambayo anasema itakuwa tofauti kabisa.
Akiongea na gazeti la The Sun Leona amesema : "On
my new album I will be rapping. I've discovered my voice for rapping.
"I could probably go up against Nicki Minaj now.
I'm actually that good, so I'm coming for you Nicki! London style MCing."
Makala: Makosa yanayofanywa na wasanii wetu wakubwa
2:04 PM
•
Rama Dee |
Na Emmanuel Msigwa aka DJ Msigwa: Radio Journalist,
Presenter ,Radio DJ & Club DJ, Pride Fm Mtwara
Nimekuwa nikiumia sana kuona wasanii wetu ambao
tunawaita wasanii wakubwa, hapa nina imani unanielewa ninaposema “wasanii
wakubwa” na nikisema nitaje majina nahisi orodha itakuwa ndefu lakini leo
naomba nimtaje mmoja ambaye amekuwa sehemu ya wasanii ambao wanazikosea sana
kazi zao hasa video za nyimbo zao na nitaeleza wapi wanakosea,nini wanatakiwa
kufanya ili muziki wetu uweze kusonga mbele zaidi ya hapa ulipofikia.
Leo naomba nianze na RAMA DEE, huyu ki ukweli ni mmoja
kati ya wasanii wa Tanzania ambao mimi nawaona wana vipaji vya hali ya juu
katika aina ya muziki wanaoufanya hasa wanapofanya “rhythm and blues “ yaani
r&b nani ambaye hajui sauti nzuri ya jamaa huyu? Nani hajui ngoma kali
zilizofanywa na jamaa huyu? Na ni nani pia ambaye haujui ngoma kali alizoshiriki
kuzipamba kwa sauti yake tamu? Je unaikumbuka J.O.S.E.P.H ya Prof Jay?
Unaikumbuka ngoma kama RIDHIKA NAMI,
SARA,NAJUA na SIYO WAOAJI? Bila shaka hizi si ngoma ngeni masikioni
mwako…kifupi jamaa anaweza sana mimi ni mmoja kati ya mashabiki wake!
Kwa sasa jamaa ametoka na ngoma yake mpya inayoitwa KUWA
NA SUBIRA ambayo ndani wameshirikishwa rafiki
zake wa kitambo MAPACHA, umewahi kuisikia ngoma hiyo? Kama bado sikiliza
ngoma hiyo! Ngoma haina hata mwezi toka
ilipotoka yawezekana wiki mbili tu au tatu toka ilipoachiwa, nakumbuka mimi
nilikuwa mmoja kati ya watu waliandika katika “wall” zetu za facebook
niliusifia sana wimbo huo na kwangu mimi naona MAPACHA walistahili kuwepo
katika wimbo huo.
Licha ya uzuri wa wimbo huo bado napata mashaka ubora wa
wimbo huo unaweza kuwa wa muda mrefu? Je ngoma hiyo inaweza kukaa miaka hata
kumi (10) ukahit kama ilivyo sasa? La hasha!........sidhani! nakiri tena
sidhani! Kwanini? Unaikumbuka THRILLER
ya MICHAEL JACKSON? Unajua ngoma hiyo ilitolewa mwaka gani? Kwa taarifa yako ni
kwamba mtayarishaji wa muziki aitwaye
QUINCY JONES alitengeneza ngoma hiyo kupitia album iliyopewa jina hilo mwaka
1982 je ni miaka mingapi sasa? Je umewahi kuona video ya ngoma hiyo? Bila shaka
ndiyo!......sasa basi kama haufahamu ni kwamba ubora wa video hiyo ndiyo
uliifanya ngoma hiyo kung’ara mpaka sasa kwa nini wasanii wetu hawajifunzi
kupitia wao? Je awapati nafasi ya kujifunza kupitia ngoma fulani au ndiyo
kusema wanakurupuka?
Je umepata nafasi ya kuangalia video ya wimbo huo wa
RAMA DEE wa KUWA NA SUBIRA? Ni video nzuri kwa maana ya rangi,mandhari na
uchanganyaji wake wa picha! Vipi kuhusu
wahusika? Vipi kuhusu story board ya wimbo huo? Sijui gharama ya wimbo
huo lakini nina imani tena ya dhati kabisa kuwa video hiyo itaishusha sana
thamani ya ngoma hiyo kwa maana ya audio
yake, fumba macho wakati unaisikiliza ngoma hiyo halafu wakati huo huo tazama
video yake! Je kuna uhalisia wowote? Umewahi kuusikiliza wimbo wa SAME GAL wa
R.KELLY & USHER RAYMOND? Umewahi
kuona video yake?
Si huo tu ni nyimbo nyingi sana ambazo naweza kutolea mfano
ni kweli, RAMA DEE hajui hicho? Hakuna watu wa kuwashauri wasanii wetu? Au
wasanii wenyewe hawataki kuwashirikisha watu wenye upeo wa mambo hayo?
Inasikitisha sana! Ki ukweli ngoma nyingi kali za jamaa ambao ni audio
zinaangushwa na video zake si pekee yake bali wapo wengi nitawaelezea siku
nyingine!
Wakati fulani mwaka 2011 nilipata kushiriki katika mradi
mmoja wa waandishi wa habari nchini Ujerumani na kukaa huko kwa muda kuna kitu
kimoja upande wa sanaa nilichojifunza kule moja ya vitu hivyo ni namna
wanavyosimamia kazi za sanaa na pili ni namna kazi hizo zinavyotoka mathalani
album ya msanii au wimbo wa msanii utakaoucheza klabu za disko si ule
utakaousikisiliza redioni na kadhalika ni tofauti na utakaouona katika video na
wala hautafanana na ule wewe utakaoununua tofauti uanzia katika midundo “beats”
baadhi ya mistari “lyrics” wakati
mwingine hutofautiana katika melody zake, hivyo
ndivyo wenzetu wanavyofanya kikubwa zaidi ni kwamba nyimbo zao ubebwa na
ubora wa video zake na ndiyo maana wasanii wengi wa Marekani utoa kwanza video
za nyimbo zao kabla hajasambaza audio zao.
Tungependa kuona video za wasanii wetu zibebe pia theme
ya wimbo husika, kama mtu akizungumzia suala la kumsifia mpenzi/mke wake kwa
mapishi mazuri basi tuone kipande cha muhusika akipika na si kuona anachota
maji au kuona tabasamu lake!.............ndugu zangu, rafiki zangu wasanii
badilikeni hili kazi zenu zidumu miaka hata 30 zaidi ni kuboresha video za
NYIMBO ZENU!
Naomba kuwasilisha
Jambo Squad wadai kudharauliwa na meneja.
2:00 PM
•
Jambo Squad wadai kudharauliwa na meneja eriki so ni BEEF BEEF SASA-Nigga
C aandika katika facebook "Ngoja niwaondoe utata wakazi wa Arusha au
vp! kikosi hatari cha Jambo Squad ambacho unakiona hapo kwenye picture
hatutokuwepo wala hatutofanya show cku ya tarehe 19 sheikh Amr Abeid
kwenye tamasha la Mambo Jambo radio kutokana na anataka kutulipa hela
ambayo inafaa kununulia nyanya Kilombero,,japo tumekataa lakini kuna
baadhi ya watangazaji wao wanatutangaza bado wanajidai makauzu,,,sasa
maraiya wetu mcpotuona cku hiyo msilalame kwani sisi hatotoonekana
kabisa[Music 4 lyf cyo kuuza sura]"
Subscribe to:
Posts
(
Atom
)