Home » Archives for 07/26/12
Iddi Azan: Bodi ya filamu imelala usingizi
2:22 PM
•
Mbunge wa Kinondoni Iddi Azan ameiponda bodi ya filamu
nchini kuwa imelala na hivyo kushindwa kufanya kazi yake.
Akichangia hoja bungeni kwenye mjadala wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo,
amesema zipo filamu nyingi zinazoingia nchini zenye mambo machafu lakini
hazichukuliwi hatua yoyote.
Amesema kuna mtindo umekuwa maarufu sana nchini wa
kuingizwa kwa filamu za ngono zilizotengenezwa nje lakini makava yake yakiwa na
picha za wasanii wa Tanzania.
Lisa Jensen akijitambulisha miss world
2:19 PM
•
Mwaka huu kwenye shindano la Miss World, Tanzania
inawakilishwa na aliyekuwa mshindi wa tatu kwenye Miss Tanzania 2006 Lisa
Jensen.
Shindano hilo litafanyika nchini China.
Katika video yake ya kujitambulisha iliyowekwa kwenye
akaunti ya Youtube ya Miss World anasikika akisema, “I am raising three
beautiful children back at home.” Ni sentesi ambayo imeanza kuleta mkanganyiko.
“Did she say she is raising three children?”
ni ujumbe ulioandikwa chini ya video hiyo na mtu aliyeiangalia.
Sentesi hiyo inaleta mkanganyiko kwakuwa
haieleweki kama anaamaanisha analea watoto watatu wa kwake mwenyewe ama wadogo
zake, ndugu zake, watoto yatima ama!!
Godzilla auponda mfumo wa elimu Tanzania
2:10 PM
•
Rapper mwenye swagga za 50 Cent, Godzilla ameukosoa
mfumo wa elimu uliopo nchini ambao anadai hautengenezi wataalam. Kupitia
mtandao wa Facebook, Godzilla ameandika:
Mfumo wa Elimu Tanzania inabidi ubadilishwe. Elimu ndefu
sana na haiko katika kutengeneza wataalam(Experts).
Mfano mtu kasoma hadi darasa la 7 akafeli na mtu
aliyesoma hadi Form6 akafeli wote wanakuwa sawa coz hawaajiliwi #so miaka yote
imepotea bure.
Zamani kulikuwa hadi na la 4 la mkoloni wazee wakifika la
4 wanamaliza sa hivi aje wazee?!
Fanyeni mfumo mzuri wa Elimu ili tuwe na wasomi wengi.
Updates:IGP wa Uganda aamrisha passport ya Chameleone irudishwe haraka
2:08 PM
•
Mkuu wa jeshi la polisi nchini Uganda, IGP, Kale Kayihura amewaagiza maofisa wa
Tanzania kuirudisha haraka passport ya Jose Chameleone.
Kayihura ametoa amri hiyo alipokutana na Chameleon kwenye
kituo cha polisi cha Muyenga mchana wa leo jijini Kampala.
Amesema maafisa wa hapa nchini wamesema passport ya msanii
huyo ingewasili baadaye leo na kukabisdhiwa kwake mara moja.
Leo Jose Chameleone akiwa na mashabiki wake wameandamana
kwenye ubalozi wa Tanzania nchini Uganda kudai arudishiwe passport hiyo
iliyokuwa ikishikiliwa na Erick Shigongo kwa madai kuwa meneja wake amemtapeli
dola 3500.
HIKI NDICHO ALICHOANDIKA JOSE CHAMELEONE KWENYE FB YAKE KUHUSIANA NA TUHUMA ZA ERIC SHIGONGO KUSHKILIA PASSPORT YAKE!
HAYA NDIO MANENO 240 ALIYOYASEMA DIAMOND PLATNUMS KUMALIZA MJADALA NA BABA YAKE
2:03 PM
•
.
Baada
ya stori kuandikwa kwenye magazeti kwamba Staa Diamond Platnums
anadaiwa kumtelekeza baba yake na hamjali wala hataki kusikia stori
zake, hii ndio kauli ya Diamond kuhusu hiyo ishu.
Amesema
“kiukweli ni vitu ambavyo mimi vimenishangaza sana kwa sababu sijui
chochote nakuja kukuta tu kwenye magazeti, na nisingependa nisikie
swala la mzazi wangu kusema mimi ni mtoto wake sijui nini na nini
kwamba mimi nafanya starehe sihusiki na yeye sio kauli nzuri kiukweli,
ina maana ananijua kwamba mimi ni mwanae baada ya kuwa DIAMOND”
Kwenye
line nyingine Diamond amesema “siku zote kama alijua mimi ni mtoto
wake basi angenisomesha na kunipa elimu nzuri lakini siku zote
nilihangaika na Mama yangu mzazi akanikuza na kunisomesha kwa shida na
tabu zote mpaka leo nimekua hivi, nisingependa kumsikia mtu yeyote
anaongea kwamba mimi ni mtoto wake au yeye ni nani kwa sababu siku zote
hawakuonekana, wasitake kuonekana kipindi cha Maslahi mtu ndio
anajifanya anahusika sana na mimi kama mtoto wake”
“Haya
mambo nilianza kuyasema toka natoa single ya binaadam sikujua hata
kama leo ningekuja kuwa na Prado, makazi au kuwa na haya mafanikio
mengine, baba yangu ataendelea kuwa baba yangu tu ila siwezi kumpa
kipaumbele kama ninachompa mama yangu kwa sababu kama angetaka hilo
angenijali toka mapema” – DIAMOND.
Subscribe to:
Posts
(
Atom
)