kama ulimiss Fidstyle Friday week 16 hii hapa

2:03 PM

ALAWI JUNIOR - NAKUPENDA WEWE (Official HD Video)

1:58 PM

Halima ft Rap Damu - Nimezama (Official Video)

1:56 PM

CAMP MULLA BIOGRAPHY

1:53 PM
Camp Mulla (2-5-4Low) is a newly formed entertainment group that strives to lead the local music scene to new heights. It specializes in hip hop , but has recently began branching out into different genres ranging from House/Electro, to R&B.
It is made up of three recording artistes, a producer and manager all under the Sub-Sahara Limited record Label. Although unsigned, Camp Mulla strives to always produce and give out the best in music.


Name: Marcus Kibuksoya
Stage Name: K’ Cous
Position: Head Producer , Song Writer
Age: 20
K Cous is known for his musical expertise; being the groups multi talented producer, he definitely takes a lot of credit for the groups current and upcoming success. The seriousness he puts into his work clearly reflects on to the impressive tracks he has produced.

Name: Mathew Wakhungu
Stage Name: Taio Tripper
Position: Rapper , Song Writer
Age: 18
A Co-Founder & cocky rapper is most famously known for his innovative compositions, claiming to have “the future in his hands” and being “allergic to defeat”. It’s therefore not surprising that he’s the group’s main songwriter. In the studio, he is notorious for putting one hundred and ten percent into his work, and when outside the studio, he’s busy being a top prefect and leader in high school, getting much respect and encouragement from his peers. Furthermore he is a perfectionist in all he does including his song writing and vocal passing.

Name: Michael Mutooni
Stage Name: Mykie Toni
Position: CEO & Hype-Man  
Age: 21
Also known as ‘Tuchi’ , the group looks up to him as their keystone social-media connector. Like a plug, he connects all Camp Mulla’s social networking with the fans. His business savvy attitude enables him to make choices and decisions that better the group and put them in a good market position.

Name: Karun Mungai
Stage Name: Miss Karun
Position: Lead vocalist , Song Writer
Age: 18
The vocals of Miss Karun are definitely at the level of professionals. She sings effortlessly, radiating confidence and passion for what she does. Music is definitely her forte. Her high vocal range makes her a force to reckon with and her pitch is flawless. Definitely a rising star, and one to keep your eye on.

Name: Benoit Kanema
Stage Name: Shappa Man
Position: Rapper , Song Writer
Age: 18
A Co-Founder & the group’s first rapper, Shappa Man is more than exceptionally talented. With a raspy unique and more than catchy voice, he steals the crown for most entertaining, where his extreme punch lines hit the jackpot. His personality is incorporated into his rhymes, eluding confidence and swag. To say he is lyrically gifted would be an understatement, he has a endowment that not many have – creativity and incredibility. His witty banter puts him at the top of the game, daring anyone to advance

NYUMBA ALIYOPANGA RAISI OBAMA MIAKA YA 80 SASA YAPANGISHWA KWA USD 2400

12:18 PM



(Officiall video) HUSSEIN MACHOZI - ADDICTED

7:44 AM

Muuaji aliyeua watu 12 kwenye uzinduzi wa movie ya Batman alitumia madawa yaliyomuua star wa Batman, Heath Ledger

7:42 AM


James Holmes muuaji wa watu 12

Mpaka mwaka mmoja uliopita James Eagan Holmes alionekana mwananchi wa kawaida tu wa Marekani. Kijana mzuri kabisa.
Mpenda michezo, mtu wa familia, msomi, kijana kutoka jiji la San Diego, California, alionekana kuwa na mambo makubwa mbele.
‘Alikuwa akiosha gari la wazazi wake, alicheza soka’ alisema Tom Mai, ambaye ni jirani wa familia ya Holmes kwa miaka 15.
 ‘Tulikuwa tukinywa pamoja wakati wa Christmas na aliwapa ‘cookies’ wanangu, alikuwa kijana wa kawaida wa kimarekani. Hakukuwa na kitu kibaya kwake.’ 

Alipona chupuchupu: Marcus Weaver akonesha majeraha ya risasi mkononi
Vilio
Eneo la tukio
Silaha aliyotumia
Juzi, Holmes, 24, akiwa na silaha nzito ikiwemo Remington shotgun, gobole aina ya AR-15 na zingine, aliamua kuyakatisha maisha ya wapenzi 12 wa filamu waliokuwa wameenda kutazama tolea jipya la filamu ya Batman huko Denver, Colorado.
Akiwa amedhamiria kumaliza kila aliyekuwa mbele yake na bila huruma hata chembe, Holmes aliwaua watu 12 akiwemo mtoto mdogo mwenye miaka sita, Veronica Moser. 

Jessica Ghawi miongoni mwa waliouawa
Pia aliwapa majeraha ya kudumu watu wengine 59, akiwemo mtoto mchanga mwenye miezi mitatu.
Baada ya kukamatwa mtu huyo alisema yeye ni Joker! Adui mkubwa wa  Batman, hakuna kingine! Akili yake ilikuwa inamtuma kuwa hapo alikuwa ndani ya movie hiyo. Punguani,bila shaka!
Juzi tena yakaibuka mengine kuhusu muuaji huyu kwamba mapema mwezi huu alikuwa amejiandikisha kwenye mtandao wa kutafuta wachumba wa AdultFriendFinder na akaandika kuwauliza wanajamvi “Mtanitembelea jela? (‘Will you visit me in prison?’) 


Kuna ripoti kuwa mama yake Arlene na baba yake Robert, meneja wa kampuni ya software anayeishi kwenye nyumba ya vyumba vinne  alijua tu bila hata kuuliza kuwa mtoto wake ndiye aliyehusika baada ya kusikia maujia hayo ya juzi Ijumaa.

Wazazi wake walikuwa wanajua kinachoendelea kwa mtoto wao huyo tangu mwaka jana. Alikuwa akipendelea kutembelea mitandao ya  ngono, akitumia madawa na kuwaacha majirani wa mjini mdogo wa Aurora uliopo jijini Denver na ishara kuwa kijana huyu alikuwa na matatizo makubwa.

Polisi wanaamini kuwa kijana huyo alikuwa amekuwa mlevi wa filamu za Batman na kuna ripoti ambazo bado hazijathibitishwa kuwa alijikuta akitumia sana dawa za kupunguza maumivu za Vicodin, ambazo zilikutwa kwenye mfumo wa damu wa muigizaji marehemu Heath Ledger, ambaye aliigiza kama Joker kwenye filamu ya Batman. Ledger alifariki kutokana na overdose mwaka 2008.
Mashuhuda

Hadharani, angalau wazazi wa Holmes hawasemi iwapo wanafahamu ama kukisia nini kilimfanya mtoto wao achukue uamuzi huo.

Watalaam, wanaamini kuwa Holmes alikuwa na tatizo la kisaikolojia ambalo lingekuja kulipuka katikati ya miaka 15 na 25.

Holmes alianza kusoma PhD ya neuroscience kwenye chuo kikuu cha dawa cha Colorado mjini Denver mwaka jana lakini aliacha mwezi uliopita.

Kozi ya mwisho aliyoichukua ilikuwa ni ya magonjwa ya akili na psychiatric disorders.

Awali alisoma kwenye chuo kikuu cha California ambako alipata first-class kwenye degree ya neuroscience.

Mkuu wa chuo hicho, Timothy White alisema Holmes alikuwa mwanafunzi mwenye akili.
Rais Obama akiwakumbuka marehemu siku ya ijumaa
Licha ya kuwa na shahada Holmes alilazimika kutafuta kazi kwenye mgahawa wa McDonald wa eneo analoishi baada ya kuhitimu mwaka 2010.
Mr Mai alisema: ‘Hakupata kazi hivyo aliamua kurudi shule kusomea udaktari wa falsafa.
Juzi usiku mama yake Holmes aliungana na mama yake nyumbani kwao San Diego ambako kulikuwa kumefurika waandishi wa habari. Baba yake aliwasili Colorado na kupelekwa jela aliyowekwa mwanae ambaye alikuwa amewekwa peke yake kwa usalama wake mwenyewe.
July 5 mwaka huu, Holmes alifundua akaunti kwenye mtandao huo wa kutafuta wachumba kwa jina la ‘ClassicJimbo’. 

Mama yake na Michael Jackson apotea, hajulikani alipo

7:30 AM



Mtandao wa TMZ umeripoti kuwa mama yake na hayati Michael Jackson, Katherine hajulikani alipo.

Mtoto wa Michael Paris Jackson amethibitisha taarifa hizo kwa kutweet, "yes, my grandmother is missing. I haven't spoken with her in a week I want her home now."

 Aliendelea kuandika na kuwaomba watu ama mamlaka zifuatilie: "the same doctor that testified on behalf of dr murray saying my father was a drug addict (a lie) is caring for my grandmother... just saying."

Mwanasheria wa Katherine Jackson ameiambia CNN kuwa hajaonekana ndani ya saa 24 sasa wala kuwasiliana na wajukuu zake.

Kuna taarifa ya kuwepo kwa ugomvi mkubwa kwenye familia hiyo uliosababishwa na malumbano juu ya nyumba ya Michael kiasi cha kumfanya mama yake apatwe kiharusi cha kati.

Kweli Tanzania hakuna Pesa?: Huyu ndiye Mtanzania anaemiliki Gari la Tsh Bilioni Moja

7:08 AM
Daveis mosha



“HII sasa ni kufuru!” Hivi ndivyo utakavyoweza kusema kwa Davies Mosha ambaye ni makamu mwenyekiti wa zamani wa klabu ya Yanga, ambaye nafasi yake kwa sasa klabuni hapo inashikiliwa na Clement Sanga.
Kwa tafsiri ya haraka, yawezekana Mosha anaweza kuwa ndiye kiongozi pekee wa soka nchini kumiliki gari la kifahari na lenye gharama kubwa aina ya Lamborghini kama ambalo linamilikiwa na mshambuliaji wa Manchester United, Wayne Rooney.
Gari analomiliki Mosha ambalo lina rangi ya njano, linaaminika kuwa miongoni mwa magari yenye thamani kubwa siyo tu Tanzania na Afrika, bali duniani kote, kwani hata siku Rooney alipolinunua wenzake wengi hawakutegemea, siyo kwa sababu hana fedha, ila kwa kuwa hakuwa mtu wa matumizi ya magari yenye thamani kubwa kama hilo.
Mosha ameliambia Championi Ijumaa kuwa anamiliki magari kadhaa ya kifahari kwa matumizi yake binafsi na familia yake.

Yafuatayo ni maelezo kuhusiana na gari hilo la kifahari kwa kuanzia kiwango cha mafuta na usumbufu anaoupata akiwa katika mizunguko yake.
Ameinunua kwa bei gani?
“Kutokana na ubora wa gari hili, nililazimika kutoa shilingi bilioni moja kwa ajili ya kulinunua, kama unavyojua ni fedha nyingi, nimenunua kwa mapenzi yangu.
Alipolinunua
“Hili gari kaniuzia mtoto wa Bakhresa (Yusuph), baada ya kufikia makubaliano kati yake na mimi, aliniuzia Julai 2011.
Spidi ya gari
“Hili gari kasi yake ya mwisho ni 360, ni kasi kali na inatosha kwa matumizi yangu binafsi.
Matumizi ya mafuta
“Matumizi ni ya kawaida wala siyo ya kuogopesha sana, inategemea na umbali utakaotembea.
Usumbufu anaoupata
“Usumbufu mkubwa ninaoupata kiukweli, nikiwa naendesha barabarani, madereva wengine wanalishangaa sana, hali inayosababisha kutokea ajali au msuguano mara kadhaa.
“Hivi karibuni dereva mmoja aliigonga sehemu ya tairi la nyuma kushoto kutokana na kuishangaa, ilikuwa maeneo ya Masaki hapahapa Dar es Salaam.
“Matengenezo yake yaligharimu pauni 20,000 (zaidi ya shilingi milioni 50), hali iliyosababisha niwe makini nikiwa naendesha,” anasema Mosha.
“Matengenezo yake yaligharimu pauni 20,000 (zaidi ya shilingi milioni 50), hali iliyosababisha niwe makini nikiwa naendesha,” anasema Mosha.
 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates