Home » Archives for 07/22/12
CAMP MULLA BIOGRAPHY
1:53 PM
•
Camp
Mulla (2-5-4Low) is a newly formed entertainment group that strives to
lead the local music scene to new heights. It specializes in hip hop ,
but has recently began branching out into different genres ranging
from House/Electro, to R&B.
It is made up of three recording artistes, a producer and manager all under the Sub-Sahara Limited record Label. Although unsigned, Camp Mulla strives to always produce and give out the best in music.
It is made up of three recording artistes, a producer and manager all under the Sub-Sahara Limited record Label. Although unsigned, Camp Mulla strives to always produce and give out the best in music.
Name: Marcus Kibuksoya
Stage Name: K’ Cous
Position: Head Producer , Song Writer
Age: 20
K
Cous is known for his musical expertise; being the groups multi
talented producer, he definitely takes a lot of credit for the groups
current and upcoming success. The seriousness he puts into his work
clearly reflects on to the impressive tracks he has produced.
Name: Mathew Wakhungu
Stage Name: Taio Tripper
Position: Rapper , Song Writer
Age: 18
A
Co-Founder & cocky rapper is most famously known for his
innovative compositions, claiming to have “the future in his hands” and
being “allergic to defeat”. It’s therefore not surprising that he’s the
group’s main songwriter. In the studio, he is notorious for putting
one hundred and ten percent into his work, and when outside the studio,
he’s busy being a top prefect and leader in high school, getting much
respect and encouragement from his peers. Furthermore he is a
perfectionist in all he does including his song writing and vocal
passing.
Name: Michael Mutooni
Stage Name: Mykie Toni
Position: CEO & Hype-Man
Age: 21
Also
known as ‘Tuchi’ , the group looks up to him as their keystone
social-media connector. Like a plug, he connects all Camp Mulla’s social
networking with the fans. His business savvy attitude enables him to
make choices and decisions that better the group and put them in a good
market position.
Name: Karun Mungai
Stage Name: Miss Karun
Position: Lead vocalist , Song Writer
Age: 18
The
vocals of Miss Karun are definitely at the level of
professionals. She sings effortlessly, radiating confidence and passion
for what she does. Music is definitely her forte. Her high vocal range
makes her a force to reckon with and her pitch is flawless. Definitely a
rising star, and one to keep your eye on.
Stage Name: Shappa Man
Position: Rapper , Song Writer
Age: 18
A Co-Founder & the group’s first rapper, Shappa Man is more than exceptionally talented. With a raspy unique and more than catchy voice, he steals the crown for most entertaining, where his extreme punch lines hit the jackpot. His personality is incorporated into his rhymes, eluding confidence and swag. To say he is lyrically gifted would be an understatement, he has a endowment that not many have – creativity and incredibility. His witty banter puts him at the top of the game, daring anyone to advance
Muuaji aliyeua watu 12 kwenye uzinduzi wa movie ya Batman alitumia madawa yaliyomuua star wa Batman, Heath Ledger
7:42 AM
•
James Holmes muuaji wa watu 12 |
Mpaka mwaka mmoja uliopita James Eagan Holmes alionekana
mwananchi wa kawaida tu wa Marekani. Kijana mzuri kabisa.
Mpenda michezo, mtu wa familia, msomi, kijana kutoka jiji la
San Diego, California, alionekana kuwa na mambo makubwa mbele.
‘Alikuwa akiosha gari la wazazi wake, alicheza soka’ alisema
Tom Mai, ambaye ni jirani wa familia ya Holmes kwa miaka 15.
‘Tulikuwa tukinywa
pamoja wakati wa Christmas na aliwapa ‘cookies’ wanangu, alikuwa kijana wa
kawaida wa kimarekani. Hakukuwa na kitu kibaya kwake.’
Alipona chupuchupu: Marcus Weaver akonesha majeraha ya risasi mkononi |
Vilio |
Eneo la tukio |
Silaha aliyotumia |
Juzi, Holmes, 24, akiwa na silaha nzito ikiwemo Remington
shotgun, gobole aina ya AR-15 na zingine, aliamua kuyakatisha maisha ya wapenzi
12 wa filamu waliokuwa wameenda kutazama tolea jipya la filamu ya Batman huko
Denver, Colorado.
Akiwa amedhamiria kumaliza kila aliyekuwa mbele yake na bila
huruma hata chembe, Holmes aliwaua watu 12 akiwemo mtoto mdogo mwenye miaka
sita, Veronica Moser.
Jessica Ghawi miongoni mwa waliouawa |
Pia aliwapa majeraha ya kudumu watu wengine 59, akiwemo
mtoto mchanga mwenye miezi mitatu.
Baada ya kukamatwa mtu huyo alisema yeye ni Joker! Adui
mkubwa wa Batman, hakuna kingine! Akili
yake ilikuwa inamtuma kuwa hapo alikuwa ndani ya movie hiyo. Punguani,bila
shaka!
Juzi tena yakaibuka mengine kuhusu muuaji huyu kwamba mapema
mwezi huu alikuwa amejiandikisha kwenye mtandao wa kutafuta wachumba wa
AdultFriendFinder na akaandika kuwauliza wanajamvi “Mtanitembelea jela? (‘Will
you visit me in prison?’)
Kuna ripoti kuwa mama yake Arlene na baba yake Robert, meneja
wa kampuni ya software anayeishi kwenye nyumba ya vyumba vinne alijua tu bila hata kuuliza kuwa mtoto wake
ndiye aliyehusika baada ya kusikia maujia hayo ya juzi Ijumaa.
Wazazi wake walikuwa wanajua kinachoendelea kwa mtoto
wao huyo tangu mwaka jana. Alikuwa akipendelea kutembelea mitandao ya ngono, akitumia madawa na kuwaacha majirani
wa mjini mdogo wa Aurora uliopo jijini Denver na ishara kuwa kijana huyu
alikuwa na matatizo makubwa.
Polisi wanaamini kuwa kijana huyo alikuwa amekuwa mlevi
wa filamu za Batman na kuna ripoti ambazo bado hazijathibitishwa kuwa alijikuta
akitumia sana dawa za kupunguza maumivu za Vicodin, ambazo zilikutwa kwenye
mfumo wa damu wa muigizaji marehemu Heath Ledger, ambaye aliigiza kama Joker
kwenye filamu ya Batman. Ledger alifariki kutokana na overdose mwaka 2008.
Mashuhuda |
Hadharani, angalau wazazi wa Holmes hawasemi iwapo
wanafahamu ama kukisia nini kilimfanya mtoto wao achukue uamuzi huo.
Watalaam, wanaamini kuwa Holmes alikuwa na tatizo la
kisaikolojia ambalo lingekuja kulipuka katikati ya miaka 15 na 25.
Holmes alianza kusoma PhD ya neuroscience kwenye chuo
kikuu cha dawa cha Colorado mjini Denver mwaka jana lakini aliacha mwezi
uliopita.
Kozi ya mwisho aliyoichukua ilikuwa ni ya magonjwa ya
akili na psychiatric disorders.
Awali alisoma kwenye chuo kikuu cha California ambako
alipata first-class kwenye degree ya neuroscience.
Mkuu wa chuo hicho, Timothy White alisema Holmes alikuwa
mwanafunzi mwenye akili.
Rais Obama akiwakumbuka marehemu siku ya ijumaa |
Licha ya kuwa na shahada Holmes alilazimika kutafuta kazi
kwenye mgahawa wa McDonald wa eneo analoishi baada ya kuhitimu mwaka 2010.
Mr Mai alisema: ‘Hakupata kazi hivyo aliamua kurudi shule
kusomea udaktari wa falsafa.
Juzi usiku mama yake Holmes aliungana na mama yake nyumbani
kwao San Diego ambako kulikuwa kumefurika waandishi wa habari. Baba yake
aliwasili Colorado na kupelekwa jela aliyowekwa mwanae ambaye alikuwa amewekwa
peke yake kwa usalama wake mwenyewe.
July 5 mwaka huu, Holmes alifundua akaunti kwenye mtandao
huo wa kutafuta wachumba kwa jina la ‘ClassicJimbo’.
Mama yake na Michael Jackson apotea, hajulikani alipo
7:30 AM
•
Mtandao wa TMZ umeripoti kuwa mama yake na hayati Michael
Jackson, Katherine hajulikani alipo.
Mtoto wa Michael Paris Jackson amethibitisha taarifa hizo kwa
kutweet, "yes, my grandmother is missing. I haven't spoken with her in a
week I want her home now."
Aliendelea kuandika na
kuwaomba watu ama mamlaka zifuatilie: "the same doctor that testified on
behalf of dr murray saying my father was a drug addict (a lie) is caring for my
grandmother... just saying."
Mwanasheria wa Katherine Jackson ameiambia CNN kuwa
hajaonekana ndani ya saa 24 sasa wala kuwasiliana na wajukuu zake.
Kweli Tanzania hakuna Pesa?: Huyu ndiye Mtanzania anaemiliki Gari la Tsh Bilioni Moja
7:08 AM
•
Daveis mosha |
“HII
sasa ni kufuru!” Hivi ndivyo utakavyoweza kusema kwa Davies Mosha
ambaye ni makamu mwenyekiti wa zamani wa klabu ya Yanga, ambaye nafasi
yake kwa sasa klabuni hapo inashikiliwa na Clement Sanga.
Kwa
tafsiri ya haraka, yawezekana Mosha anaweza kuwa ndiye kiongozi pekee
wa soka nchini kumiliki gari la kifahari na lenye gharama kubwa aina ya
Lamborghini kama ambalo linamilikiwa na mshambuliaji wa Manchester
United, Wayne Rooney.
Gari
analomiliki Mosha ambalo lina rangi ya njano, linaaminika kuwa miongoni
mwa magari yenye thamani kubwa siyo tu Tanzania na Afrika, bali duniani
kote, kwani hata siku Rooney alipolinunua wenzake wengi hawakutegemea,
siyo kwa sababu hana fedha, ila kwa kuwa hakuwa mtu wa matumizi ya
magari yenye thamani kubwa kama hilo.
Mosha ameliambia Championi Ijumaa kuwa anamiliki magari kadhaa ya kifahari kwa matumizi yake binafsi na familia yake.
Yafuatayo
ni maelezo kuhusiana na gari hilo la kifahari kwa kuanzia kiwango cha
mafuta na usumbufu anaoupata akiwa katika mizunguko yake.
Ameinunua kwa bei gani?
“Kutokana
na ubora wa gari hili, nililazimika kutoa shilingi bilioni moja kwa
ajili ya kulinunua, kama unavyojua ni fedha nyingi, nimenunua kwa
mapenzi yangu.
Alipolinunua
“Hili gari kaniuzia mtoto wa Bakhresa (Yusuph), baada ya kufikia makubaliano kati yake na mimi, aliniuzia Julai 2011.
Spidi ya gari
“Hili gari kasi yake ya mwisho ni 360, ni kasi kali na inatosha kwa matumizi yangu binafsi.
Matumizi ya mafuta
“Matumizi ni ya kawaida wala siyo ya kuogopesha sana, inategemea na umbali utakaotembea.
Usumbufu anaoupata
“Usumbufu
mkubwa ninaoupata kiukweli, nikiwa naendesha barabarani, madereva
wengine wanalishangaa sana, hali inayosababisha kutokea ajali au
msuguano mara kadhaa.
“Hivi
karibuni dereva mmoja aliigonga sehemu ya tairi la nyuma kushoto
kutokana na kuishangaa, ilikuwa maeneo ya Masaki hapahapa Dar es Salaam.
“Matengenezo
yake yaligharimu pauni 20,000 (zaidi ya shilingi milioni 50), hali
iliyosababisha niwe makini nikiwa naendesha,” anasema Mosha.
“Matengenezo
yake yaligharimu pauni 20,000 (zaidi ya shilingi milioni 50), hali
iliyosababisha niwe makini nikiwa naendesha,” anasema Mosha.
Subscribe to:
Posts
(
Atom
)