Ni nani huyu aliyempagawisha Diva hivi?

1:23 PM



Okay, umpende usimpende, Loveness aka Diva ni mtangazaji anayezungumzwa zaidi nchini. Ukianzia kwenye kipindi chake mpaka maisha ya kawaida, ni full of drama.

Mwezi uliopita alitoa ngoma yake ‘Piga Simu’ akiwa na Diamond na imepata promo ya nguvu husasan kwenye kituo anachofanyia kazi, Clouds Fm, si unajua mcheza kwao hutuzwa!

Well, kisa cha wimbo huo ni kwamba jamaa yake ni mtu wa mishemishe sana kiasi ambacho anakuwa hana muda wa kutulia sehemu naye na kuenjoy mahaba yao. Inaonekana ni mtu fulani hivi mambo safi sababu jamaa ni mzee wa kukwea pipa kwa sana.

So ndo Diva akaamua kuandika wimbo huo kumtaka walau ampigie simu ili japo asikie tu sauti yake. Tangu atoe wimbo huo, kwenye page yake ya Twitter pamoja na kuandika mambo mengine, amekuwa akiandika ujumbe mwingi kuonesha ni kiasi gani anamzimia mchizi huyo.

Na pia kwa sasa amesharekodi wimbo mwingine uitwao ‘Mgonjwa kwa raha zako’ maalum kwaajili ya jamaa huyu huyu. So who the hell is this guy? Kampa nini mtoto wa watu mbona kadata hivi?

“I love u so much, God knows how much I do love u, its only u , tried to think of u in every step I take, My heart stuck with only u,” aliandika wiki hii.
“Hope one day u will understand how much I truly love u, whatever u do jus kno that I love you,”

“Been in love with u completely. I love ma baby .....so in love with him , I lovE ma baby ‪#singing.”

“Mwinginewe achomozi nakupenda peke yako , Daima nitakuenzi silitupi Pendo lako. Naingia simanzi kukukosa siwezi...Wallah sijitambui mgonjwa kwa raha zako ......

Nakesha macho kwa kutia toba ...... Kofi zito limenizaba kisa mahaba ... Ananionea eeh???

Nakonda na kukosa haiba ..... Kisa kupenda, macho yameziba kisa mahaba , ..... ♥♥

Na ili kuonesha kuwa baadhi ya maneno hayo yatasikika kwenye wimbo wake aliandika, “Lile busu Pembeni ya bahari , na ule upepo mwanana nakupenda sina hali .... Finishing mgonjwa kwa raha zako at Fishcrab.”

Anyway shout outs to the dude! He is good.

Ray azindua ‘Sobbing Sound’ kwa kusaidia yatima

1:13 PM


Muigizaji maarufu wa nchini Tanzania Raymond Kigosi weekend hii amezindua filamu yake mpya iitwayo Sobbing Sound kwa kuendana na shughuli za kutoa msaada kwa watoto yatima.

Kupitia blog yake Ray ameandika, “Hatimaye mzigo wa Sobbing Sound umeingia mtaani kwa aina yake baada ya kaumua kwenda kuuzindua na watoto yatima wa kituo cha Maunga kilichopo maneno ya Kinondoni studio.”
Amesema ameamua kufanya hivyo baada ya kuguswa na jinsi watoto yatima wanavyoishi katika mazingira magumu.

Ray akikabidhi misaada
Ray akiwa pamoja na watoto yatima
“Hili ni jukumu la watanzania wote kuanza kuguswa katika hili maana hapa duniani sisi ni wapangaji tu makazi yetu ni kwa Mungu Baba, sasa unapopata kidogo jaribu kuwafikiria na wale waliokuwa na maisha magumu, yani tugawane umasikini.”

Aliongeza kwa kusema, “sikuwa na kikubwa sana ila nimejitolea pale nilipoweza kubarikiwa na Mungu Baba. Unaambiwa kuwa kama hutoweza kushukuru kwa kidogo basi hata ukipata kikubwa pia utakuwa mgumu kumshukuru yule aliyekuwezesha kukupa kipato hicho.”


Filamu ya Sobbing Sound imetoka chini ya kampuni ya Steps Entertainment na ameigiza .

Bob Junior atengeneza ‘mshiko’ kwa njia ya harus

1:08 PM

Hauhitaji degree ili upate hela nyingi kwenye muziki, ni akili na ubunifu tu. Jana rais wa masharobaro, Bob Junior aka Mr. Chocolate Flava, amefunga ndo kwa style yake na kudhihirisha kuwa, msanii anaweza kuingiza hela kwa mgongo wa harusi. Sio kwa michango ya ndugu by the way, ni kwa mashabiki kwenda kulishuhudia jiko lake na pia kuburudika na show ya nguvu kwa kulipa kiingilio.


Producer huyo aliyemtambulisha Diamond na kumtoa kimuziki, aliamua kuua ndege wawili kwa jiwe moja kwa kuunganisha harusi yake na show yake ya jana ya Bilicanas.
Kwa kiongilio cha shilingi elfu sita tu mlangoni, mashabiki wake waliweza kumshuhudia mke wake aliyemtoa Zanzibar. What a wedding!



Awali kabla ya kurejea Dar, Bob Junior alihakikisha pia anachukua hela za wazanzibar katika show aliyoipiga kujitambulisha ‘ukweni.’
Kwenye show hiyo iliyoitwa, “Nichumu, Nikiss Mwaah Nite” iliyofanyika Ngome Kongwe Zanzibar, watu kibao walijitokeza kumuangalia akikata mauno kama kawaida yake na baadaye kumpandisha mke wake stejini.


Miongoni mwa wasanii waliompa tafu kwenye show hiyo ya Zanzibar ni pamoja na Queen Darleen na Cassim.
 

Wow! That was a sellout show!  Hongera Bob.

THE MAKING OF MUSIC VIDEO AIFORA by LINEX

12:38 PM

Congrats to Nicholaus Haule a.k.a Black Rhino and Beatrice Mbaga Haule on Your Wedding Day

12:34 PM



    
Ni zaidi ya miaka kama 8 hivi toka niwaone mkiwa wote Black Rhino & Beatrice, sasa ile ndoto yenu imekamilika jumamosi hii iliyopita ya tarehe 1. Mungu awabariki muendelee kuwa pamoja hivyo hivyo mpaka kifo kitakapo kuja kuwatenganisha ndugu zangu. Na mimi nawaahidi kufuata nyayo zenu, ingawa sikuwepo katika sherehe yenu kwa kuumwa basi naimani moyo wangu upo nanyi siku zote.


FID Q FT Yvonne mwale - SIHITAJI MARAFIKI

12:15 PM

 
Copyright © CHIWILEINC. Designed by OddThemes | Distributed By Gooyaabi Templates